Ijumaa, 24 Aprili 2015

Wahamiaji:Wanahabari wa UK washtumiwa

  • Saa 4 zilizopita
Mkuuwa haki za kibinaadamu katika umoja wa mataifa
Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Zeid Ra’ad Hussein, amekuwa akifadhaishwa sana na lugha ya magazeti ya Uingereza wanayotumia dhidi ya wakimbizi, lakini ni taarifa ya hivi punde iliyochapishwa na makala ya
‘The Sun’ iliyomghadhabisha zaidi.
Makala hiyo iliwaita wakimbizi mende, matamshi ambayo Hussein anasesema ni sawia na yale yaliotumika Rwanda kabla ya mauaji ya kimbari.
Wahamiaji
Mkuu huyo wa Haki za Kibinadamu amesema taarifa hiyo ya The Sun ilikuwa mojawapo tu ya taarifa nyingi za chuki na za kibaguzi ambazo zimechapishwa kwa miongo mingi na magazeti ya Uingereza.
Alisema desturi hii ilikuwa inaongeza moto wa chuki na udhalilishaji wa binadamu wengine. Hussein alisema kuwa malalamishi kuhusu makala hizo tayari yamepelekwa kwa Polisi wa jiji na akataka kuchukuliwe hatua kali.
Wahamiaji
Matamshi haya, hasa kutoka kwa afisa wa juu sana wa umoja wa mataifa, umeashiria wasiwasi ulioko kuhusu mjadala unaoendelea bara Uropa kuhusu wakimbizi wanaovukia Meditteranean kuingia Ulaya .
Mjadala ambao unasemekana unaendeshwa na hisia kali kwenye vyombo vya habari, na kwamba maoni ya uma huenda hayaungi mkono hatua zinazohitajika kuokoa maisha ya wanaokufa maji huko mediterrenean

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni